Monday, August 26, 2013

PELLEGRINI ALAUMU SAFU YAKE YA ULINZI KWA KUKOSA UMAKINI.

MENEJA wa klabu ya Manchester City, Manuel Pellegrini amelaumu uwezo wa safu yake ya ulinzi kushindwa kuzuia mipira miwili ya kona na kupelekea timu yake kupata kipigo cha kushangaza cha mabao 3-2 kutoka kwa timu iliyopanda daraja msimu huu ya Cardiff City. Pellegrin amesema kitu kibaya zaidi walitangulia kuondoza naa baada ya kushinda bao hilo alitegemea mambo kuwa rahisi kwao lakini mipira miwili ya kona kutoka kwa wapinzani wao iliamua matokeo hayo. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa hakutegemea kufungwa katika mchezo huo lakini kwa jinsi wapinzani wao walivyokuwa wakijilinda iliwawia vigumu kwao kutengeneza nafasi za kufunga. Lakini kocha huyo amesema pamoja na kipigo hicho walichopata hawatakiwi kukata tamaa kwani ligi bado ndefu na taratibu watajaribu kurejesha makali yao ili waweze kufanya vyema katika mechi ijayo dhidi ya Hull City.

No comments:

Post a Comment