Monday, August 26, 2013

ZUBIZARRETA AMUUNGA MKONO MARTINO KUMPUMZISHA NEYMAR.

MKURUGENZI wa michezo wa klabu ya Barcelona, Andoni Zubizarreta anamuunga Gerardo Martino jinsi anavyolishughulikia suala la Neymar ambapo kocha huyo amekuwa akitumia muda mwingi kumpumzisha mchezaji huyo. Kwa mara nyingine Neymar alipangwa kama mchezaji wa akiba katika ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Malaga pamoja na kuumia kwa Lionel Messi ambaye hakucheza katika mechi hiyo ya jana. Pamoja na Messi kuumia Zubizarreta anaamini kuwa Martino alichukua uamuzi sahihi kutomuanzisha katika mechi hiyo kwasababu bado hajakuwa fiti kucheza dakika zote tisini kutokana na kutopumzika kwa muda wa kutosha. Zubizarreta amesema nyota huyo atakuwepo hapo kwa kipindi kirefu hivyo mashabiki watapata nafasi ya kumuona akicheza dakika 90 wakati akiwa fiti kwa asilimia 100. Neymar ambaye amejiunga na Barcelona akitokea Santos kwa ada ya euro milioni 57 mapema masimu huu, aligundulika na tatizo la upungufu wa damu kabla ya kupoteza uzito wa kilo saba baada ya kufanyiwa upasuaji wa koo wa maandalizi ya msimu mpya.

No comments:

Post a Comment