Tuesday, August 27, 2013

MOURINHO AMPA ROONEY SAA 48 ZA KUCHAGUA.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amempa Wayne Rooney saa 48 kuchagua kama anataka kuondoka Manchester United na kwenda Stamford Bridge. United imekuwa ikisisitiza kuwa hawana mpango wa kumuuza nyota wake huyo ambaye alionyesha mchezo wa hali ya juu katika mechi baina ya timu hizo iliyoisha kwa sare ya bila kufungana jana. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Mourinho amesema mtu aliyeanzisha habari hiyo ndio anatakiwa kumaliza na muda wa kufanya hilo umefika. Mourinho amesema Rooney anatakiwa kutamka kwa kinywa chake kama anataka kuondoka au kubakia Old Traford kwa msimu mwingine.

No comments:

Post a Comment