Thursday, August 22, 2013

FIFA YAPATA MAOMBI ZAIDI MILIONI 2.3 YA TIKETI KATIKA SAA 24 ZA KWANZA TOKA ZIINGIE SOKONI.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limedai kuwa zaidi tiketi milioni 2.3 zimeombwa na mashabiki kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia 2014 katika saa 24 za kwanza toka ziwekwe sokoni katika mtandao. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wake FIFA imesema toka tiketi hizo ziingie sokoni kwa mara ya kwanza zaidi ya mashabiki 400,000 wametuma maombi ya zaidi ya tiketi milioni 2.3. FIFA imesema maombi mengi ya tiketi hizo yametoka katika nchi za Brazil ambao ndio wenyeji wa michuano hiyo, Argentina, Marekani, Chile na Colombia. Kuna maombi ya tiketi zaidi ya 372,000 kwa ajili ya mechi ya ufunguzi itakayofanyika jijini Sao Paulo Juni 12 na zaidi ya maombi 344,000 kwa tiketi za mchezo wa fainali utakaofanyika katika Uwanja wa Maracana jijini Rio de Janeiro Julai 13 mwakani. Tiketi hizo zilianza kuingia sokoni Jumanne na mashabiki watatakiwa kutuma maombi yao mpaka kufikia Octoba 10 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment