Tuesday, August 27, 2013

HIGUAIN APATA AJALI YA BOTI ITALIA.

VYOMBO vya habari nchini Italia vimeripoti kuwa mshambuliaji mpya wa klabu ya Napoli, Gonzalo Higuain ameshonwa nyuzi 10 usoni baada ya kupata ajali ya boti Jumatatu. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina ameripotiwa kupata na ajali na kujigonga usoni katika boti aliyokuwa akitumia katika kisiwa cha Capri kilichopo kusini mwa pwani ya nchi hiyo. Nyota alitibiwa kusiwani humo na baadae kuruhusiwa ambapo klabu yake ambayo inakabiliwa na mechi dhidi ya Chievo Jumamosi haikuzungumzia lolote kuhusiana na tukio hilo. Higuain alijunga na Napoli akitokea Real Madrid JUlai mwaka huu na alicheza mechi ya kwanza ya Serie A dhidi ya Bologna ambapo timu yake ilishinda mabao 3-0.

No comments:

Post a Comment