Thursday, August 22, 2013

KOCHA WA DINAMO ZAGREB ATIMULIWA BAADA YA KIPIGO.

RAIS wa klabu ya Dinamo Zagreb ya Croatia, Zdravko Mamic ametangaza kumtimua kocha wake Krunoslav Jurcic baada ya kipigo cha mabao 2-0 iliyopata timu hiyo kutoka kwa Vienna ya Austria katika mechi ya mkondo wa kwanza hatua ya mtoano ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Jurcic aliiongoza Zagreb kuweka rekodi ya kushinda taji la nne mfululizo la Ligi Kuu ya nchi hiyo April mwaka huu huku wakiongoza msimamo wa ligi hiyo baada ya kucheza mechi sita lakini amejikuta akitimuliwa baada ya kipigo hicho walichopata jana usiku. Katika taarifa yake iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo, Mamic alimshukuru kocha huyo kwa alichokifanya katika kipindi cha miaka mitatu waliyokuwa nayo lakini ameamua kumuachia aondoke kwasababu ya kipigo walichopata kutoka kwa Vienna. Taarifa hiyo iliongeza kuwa msaidizi wa kocha huyo Damir Krznar ndiye atashika nafasi hiyo kwa muda mpaka hapo watakapopata mbadala mwingine katika siku chache zijazo.

No comments:

Post a Comment