Saturday, September 28, 2013

ARSENAL HAWANA UBAVU WA KUMALIZA TOP FOUR MSIMU HUU - OWEN.

MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Liverpool na Manchester United, Michael Owen anaamini kuwa Arsenal hawana kikosi chenye uwezo wa kumaliza katika nafasi nne za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini Uingereza msimu huu. Kikosi cha Arsenal kinachonolewa na Arsene Wenger kwasasa kinaongoza ligi kwa tofauti ya mabao baada ya kushinda mechi zake nne kati ya tano walizocheza msimu huu. Pamoja na hivyo Owen anaamini Arsenal hawana nafasi ya kumaliza msimu wa ligi wakiwa katika nafasi nne kutokana na aina ya wachezaji waliopo katika kikosi cha Wenger. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kama akipewa nafasi ya kuchagua wachezaji nyota wa ligi kutoka katika vilabu sita kwa Arsenal atamchukua mmoja pekee ambaye ni Mesut Ozil wengine waliobakia ni wachezaji wa kawaida. Owen amesema ukilinganisha na usajili waliofanya Chelsea, Tottenham Hotspurs na timu zingine anaona Arsenal nafasi yao itakuwa ndogo msimu huu.

No comments:

Post a Comment