Saturday, September 28, 2013

ETO'O AITWA CAMEROON PAMOJA NA KUZUSHIWA KUSTAAFU.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Cameroon, Samuel Eto’o ameitwa katika kikosi cha wachezaji 25 cha timu ya taifa ya nchi hiyo ambacho kitakwaana na Tunisia kwenye mchezo wa hatua ya mtoano pamoja na vyombo vya habari kuripoti kuwa nyota huyo amestaafu soka la kimataifa. Vyombo vya habari vya nchi viliripoti kuwa Eto’o ambaye pia ndio nahodha wa Cameroon alitangaza kustaafu soka la kimataifa kwa sababu za kifamilia katika vyumba vya kubadilishia nguo baada ya kushinda mechi yao dhidi ya Libya mapema mwezi huu. Hata hivyo Eto’o hakusema chochote kuhusiana na tetesi hizo na kocha wa Cameroon Volke Finke alipuuza tetesi hizo na kudai kuwa mshambuliaji huyo wa Chelsea mwenye umri wa miaka 32 ni mchezaji sahihi wa kukiongoza kikosi chake katika kutafuta nafasi ya kufuzu Kombe la Dunia. Mechi hiyo ya mkondo wa kwanza itapigwa katika Uwanja wa Rades jijini Tunis Octoba 13 huku ile ya marudiano ikichezwa jijini Yaounde Nevemba mwaka huu na mshindi wa jumla atafuzu michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil mwakani.

No comments:

Post a Comment