Saturday, September 28, 2013

FIFA YAILIMA ADHABU UKRAINE KWA UBAGUZI.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limetangaza kuufungia Uwanja wa Taifa wa Ukraine na pia nchi hiyo kucheza bila mashabiki katika mechi yao ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia watakayocheza nyumbani. Hatua hiyo imekuja kufuatia tukio la mashabiki wa soka wan chi hiyo kupiga kelele za kibaguzi katika mchezo baina ya timu ya taifa ya nchi hiyo na San Marino uliofanyika jijini Lviv. Katika taarifa yake, FIFA imedai kufikia hatua hiyo baada ya kujiridhisha na ushahidi wa picha za video pamoja na ule uliowasilishwa na waamuzi. Mbali na kufungiwa mashabiki kwenye mchezo unaofuata, Ukraine haitaruhusiwa kutumia uwanja wake wa taifa uliopo Lviv katika mechi zozote za kufuzu kuanzia sasa mpaka katika michuano ya Kombe la Dunia 2018. Kamati ya nidhamu ya FIFA pia imeitoza nchi hiyo euro milioni 36,000.

No comments:

Post a Comment