Saturday, September 28, 2013

MESSI AMEONYESHA USHAHIDI WA WAZI - WAKILI.

WAKILI wa mshambuliaji nyota wa Barcelona, Lionel Messi amesisitiza kuwa mteja wake huyo ameonyesha ushahidi wa wazi kuhusiana na kesi ya ukwepaji kodi inayomkabili. Kesi ya nyota huyo wa kimataifa wa Argentina ilianza kusikilizwa jana ambapo alianza kujibu tuhuma hizo za kutolipa kodi stahiki kutokana na haki ya matumizi ya picha zake. Messi anatuhumiwa kuzitumia nchi za nje ya Hispania kama Belize na Uruguay kuuza haki ya matumizi ya picha kitu ambacho ni kinyume na sheria za kodi za nchi hiyo. Baba yake Messi, Jorge ambaye alilipa kiasi cha euro milioni tano katika mamlaka ya kodi nchini humo Agosti mwaka huu, pia naye anahusishwa na kesi hiyo na wote walitoa utetezi wao kwa nyakati tofauti jana.


No comments:

Post a Comment