Tuesday, September 24, 2013

BOLT AONGEZA MKATABA MNONO NA PUMA.

BINGWA mara tatu wa michuano ya olimpiki, Usain Bolt ameongeza mkataba mpya mnono zaidi wa udhamini na kampuni ya vifaa vya michezo ya Ujerumani Puma mpaka baada ya michuano ya olimpiki 2016 jijini Rio de Janeiro. Mwanariadha huyo nyota wa mbio fupi kutoka Jamaica mwenye umri wa miaka 27 amekuwa akidhaminiwa na Puma toka mwaka 2003 na mara ya mwisho kuongeza mkataba wake na kampuni hiyo ilikuwa mwaka 2010. Mapema Bolt alidai kuwa anaweza kustaafu baada ya michuano ya 2016 lakini amebadili kauli yake siku za hivi karibuni na kudai anaweza kuendelea mwaka mmoja zaidi baada ya michuano hiyo. Bolt ameshinda medali sita za dhahabu katika michuano ya olimpiki na nane zingine katika mashindano ya riadha ya dunia mpaka sasa huku akishikilia rekodi ya kukimbia kwa kasi zaidi duniani kwenye mbio za mita 100.

No comments:

Post a Comment