Monday, September 23, 2013

DI CANIO ATIMULIWA SUNDERLAND.

KLABU ya Sunderland imemtimua kocha wake Paolo Di Canio kufuatia kichapo cha mabao 3-0 ilichopata timu hiyo kutoka West Bromwich Albion katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Uingereza uliochezwa Jumamosi iliyopita. Di Canio ambaye ni mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Italia, anaiacha Sunderland ikiwa mkiani mwa msimo wa ligi kwa kuambulia alama moja katika mechi tano walizocheza mpaka sasa. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 45 aliwajia juu wachezaji wake baada ya kipigo cha Jumamosi kwa kushindwa kujituma na kuonyesha ushirikiano pindi wawapo uwanjani hatua ambayo inapelekea kupata matokeo mabovu. Di Canio ambaye alianza kucheza soka katika Ligi Kuu nchini Italia kabla ya kuhamia ligi kuu na kucheza kwa misimu saba katika vilabu vya Sheffield Wednesday, West Hama United na Charlton Athletic alianza kazi ya umeneja katika klabu ya Swindon Town. Aliteuliwa kuwa meneja wa Sunderland Machi mwaka jana kwa mkataba wa miaka miwili baada ya Martin O’Neill kutimuliwa kipindi hicho.

No comments:

Post a Comment