Friday, September 27, 2013

FIFA YAIONYA TUNISIA.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limeionya serikali ya Tunisia kuingilia masuala ya soka baada ya waziri wa michezo wa nchi hiyo Tarek Dhiab kuliomba shirikisho hilo kuvunja uongozi wa soka wan chi hiyo. FIFA imeiataka serikali ya nchi hiyo kutoingilia masuala ya shirikisho la soka la nchi hiyo kwani watalazimika kuifungia nchi hiyo kama sheria zinavyosema. Hatua hiyo imepelekea Waziri Mkuu wa nchi hiyo Ali Laarayedh kuitisha mkutano wa dharura ambao pia utahudhuriwa na wajumbe wa shirikisho hilo pamoja na wawakilishi kutoka wizara ya michezo ili kujaribu kutatua tatizo lililopo. Mapema jana msemaji wa shirikisho la soka la nchi hiyo amesema kauli ya Dhiab inaweza kuwafanya wakafungiwa na FIFA hivyo kuzifanya timu zinashiriki michuano ya Klabu Bingwa barani Afrika na Kombe la Shirikisho kukosa nafasi ya kuendelea.

No comments:

Post a Comment