Monday, September 30, 2013

HAKUNA MPANGO WA KUMUUZA BENDER - LEVERKUSEN.

KLABU ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani imeweka wazi kuwa hawana mpango wa kumuuza kiungo wao Lars Bender baada ya ripoti kuwa nyota huyo alikuwa akiwaniwa na Arsenal. Kiungo huyo wa kimataifa wa Ujerumani amekuwa akipanda kiwango na kuwa mmoja wa wachezaji wa kutegemewa wa Leverkusen toka lipojiunga nao akitokea klabu ya 1860 Munich mwaka 2009. Mkurugenzi mkuu wa klabu hiyo Michael Reschke aliuambia mtandao wa Kicker kuwa hawana mpango wa kumuuza nyota wao huyo ambaye mkataba wake unamalizika mwaka 2017. Wakati huohuo mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Rudi Voller naye alisisitiza kuwa Leverkusen haijapata ofa kutoka klabu yoyote kwa ajili ya Bender.

No comments:

Post a Comment