Thursday, October 17, 2013

SABA BORA KATIKA ORODHA ZA FIFA KUONGOZA DROO ZA UPANGAJI RATIBA YA KOMBE LA DUNIA BRAZIL.


SWITZERLAND itakuwa mojawapo ya nchi nane zitakazoongoza droo ya ratiba ya michuano ya Kombe la Dunia 2014 itakayofanyika Desemba mwaka huu baada ya kukwea mpaka nafasi ya saba katika orodha za ubora dunia zilizotangazwa leo. Hispania, Argentina, Ujerumani, Colombia, Ubelgiji na wenyeji Brazil nao pia wataongoza droo hiyo wakiungana na Uruguay kama wakifanikiwa kuwafunga Jordan katika mechi za mikondo miwili za mtoano mwezi ujao. Kama Uruguay ikishindwa kufuzu michuano hiyo, Uholanzi ambao wanashika nafasi ya nane katika orodha hizo sambamba na Italia itachukua nafasi hiyo. Katika kanuni za Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Brazil ukijumlisha na timu saba zilizopo katika orodha za juu za shirikisho hilo ndio zitaongoza droo ya upangaji ratiba ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment