Wednesday, October 23, 2013

WEBB AKANUSHA KUTAKA KUMRITHI BLATTER.

RAIS wa Shirikisho la Vyama vya Soka vya Nchi za Amerika Kaskazini, Kati na Caribbean-Concacaf, Jeffrey Webb amekanusha tetesi kuwa anataka kuchukua kugombea nafasi ya rais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA inayoshikiliwa na Sepp Blatter. Webb amehusishwa kugombea nafasi hiyo mwaka 2015, huku Blatter akipendekeza katika mkutano uliofanyika Caribbean Jumatatu iliyopita kuwa Webb anaweza kuchukua nafasi kuchukua nafasi yake siku zijazo. Lakini Webb mwenyewe alikanusha suala hilo akidai kuwa hana mpango wa kugombea nafasi hiyo katika siku za karibuni. Blatter ambaye aiongoza FIFA toka mwaka 1998 alikuwa akizungumza kufungua mkutano wa mwaka wa Concacaf. Mwaka 2011 Blatter aliwaambia viongozi wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA kwamba kipindi hiki kitakuwa cha mwisho kwake kukalia ofisi hiyo lakini mwaka huu ameonekana kubadili uamuzi baada ya kuonyesha ishara kama anaweza kugombea kwa kipindi kingine.

No comments:

Post a Comment