Wednesday, November 27, 2013

ASAMOAH ATAMBA KUIFUNGIA GHANA MABAO KATIKA KOMBE LA DUNIA.

KIUNGO wa Juventus Kwado Asamoah ambaye hajawahi kuifungia bao lolote timu yake ya taifa ya Ghana amedai kuwa ameyatunza mabao yake kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika Brazil. Nyota huyo anataka kuisaidia Ghana kwa kufunga mabao katika michuano hiyo itakayoanza kutimua vumbi katika majira ya kiangazi mwakani. Asamoah amesema lengo lao kubwa lilikuwa ni kuhakikisha wanafuzu kwenda Brazil na baada ya kufanya hivyo sasa ni wajibu wao kuhakikisha wanafanya vyema kwenye michuano hiyo. Amesema pamoja na kushindwa kufunga bao lolote katika hatua za kufuzu anadhani sasa nafasi hiyo ataipata akiwa na timu hiyo kwenye michuano hiyo.


No comments:

Post a Comment