Thursday, November 28, 2013

MADRID INAWEZA KUFANYA VYEMA BILA RONALDO - DI MARIA.

KIUNGO mahiri wa klabu ya Real Madrid, Angel Di Maria anaamini kuwa timu hiyo imeonyesha kwamba inaweza kukua bila kuwa na nyota wao Cristiano Ronaldo baada ya kuigaragaza Galatasaray kwa mabao 4-1 kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Ronaldo hakuwepo katika mchezo huo lakini hilo halikuwa kikwazo kwa kikosi hicho kinachonolewa na Carlo Ancelotti kupata ushindi ambao ambao umewavusha mpaka katika hatua ya mtoano ya michuano hiyo. Di Maria mwenye umri wa miaka 25, ambaye alifunga bao la tatu katika mchezo huo anafikiri mchezo huo ulikuwa muhimu kwao kwasbabu umewafanya kuongoza kundi B. Madrid walicheza sehemu kubwa ya mchezo huo wakiwa pungufu baada ya beki Sergio Ramos kutolewa kwa kadi nyekundu mapema. Madrid kwasasa wanaongoza kundi B wakiwa na alama 13, saba zaidi ya Juventus wanashika nafasi ya pili na tisa zaidi ya Galatasaray na Copenhagen wanaoshika nafasi ya tatu na nne.

No comments:

Post a Comment