Thursday, November 28, 2013

VILLAS BOAS APUUZA TETESI ZA KUTIMULIWA.

MENEJA wa klabu ya Tottenham Hotspurs, Andre Villas-Boas ameponda ripoti kuwa anatakiwa kufukuzwa na kusisitiza kuwa anaungwa mkono bodi ya timu hiyo. Tetesi hizo zimekuja kufuatia Spurs kuchabangwa mabao 6-0 na Manchester City Jumapili iliyopita ikiwa ni kipigo kikubwa zaidi kupata toka walipofungwa na mabao 7-1 na Newcastle mwaka 1996. Matokeo hayo ambayo Villas-Boas ameelezea kama ya aibu, yameifanya timu hiyo kucheza mechi tatu bila kupata ushindi. Villas Boas amesema ana uhakika na bodi pamoja na wachezaji katika kikosi chake kwamba watasahau matokeo hayo na kuhakikisha wanafanya vyema katika mechi zao nyingine. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa amefanya mkutano na bodi lakini hakuona dalili zozote za kutaka kumtimua kwakuwa bado wameonyesha imani kwake.

No comments:

Post a Comment