Thursday, November 28, 2013

OFISA WA NFF AFUNGIWA MIAKA 10 KWA KULA MLUNGULA.

SHIRIKISHO la Soka nchini Nigeria-NFF limetangaza kumfungia mmoja wa maofisa wake ambaye pia ni kiongozi wa klabu kwa miaka 10 kutokana na kujihusisha na masuala ya rushwa. NFF ilimfungia Olaleye Adepoju ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya nidhamu ya shirikisho hilo kutokana na kosa la kupokea rushwa kutoka katika mojawapo ya vilabu vinashiriki Ligi Kuu nchini Nigeria. Kamati ya dharura ya NFF pia ilitoa adhabu kama hiyo kwa Dapo Lam-Adesina kutokana na tukio hilo ambapo wawili hawataruhusiwa kujishughulisha na mambo ya soka ili kupisha uchunguzi. Adepoju anatuhumiwa kupokea rushwa ya dola 9,400 kabla ya kusikilizwa kesi ya kinidhamu dhidi ya klabu ya Shooting Stars kutoka Ibadan ambao ni mji mkuu wa jimbo la Oyo.

No comments:

Post a Comment