Thursday, November 28, 2013

BAYERN YAFIKIA REKODI YA BARCELONA KATIKA CHAMPIONS LEAGUE.

MABINGWA watetezi wa michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya, Bayern Munich wameendeleza ubabe katika ligi hiyo baada ya kuicharaza CSKA Moscow ya Urusi kwa mabao 3-1 katika mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Khimki Arena. Mabao ya Bayern katika mchezo huo yalifungwa na Arjen Robben, Mario Gotze na Thomas Mueller aliyefunga kwa mkwaju wa penati. Huo unakuwa ushindi wa 10 mfululizo kwa Bayern kwenye michuano hiyo hivyo kuvunja rekodi ya mwaka 2002 iliyowekwa na klabu ya Barcelona. Bayern ambayo inanolewa na Pep Guardiola inakabiliwa na mchezo wa mwisho dhidi ya Manchester City ambao ndio utakaoamua nani atamaliza kinara katika kundi D.

No comments:

Post a Comment