Wednesday, November 27, 2013

MARTINO APONDA KIWANGO CHA WACHEZAJI WAKE.

KOCHA wa klabu ya Barcelona, Gerardo Martino ameponda kiwango cha wachezaji wake walichokionyesha katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya ambao walitandikwa mabao 2-1 na Ajax katika uwanja wa Amsterdam Arena. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Martino amesema katika kipindi cha kwanza wachezaji wake walikuwa wamepoteana kabisa hivyo kuwapa mwanya wapinzani wao kuwafunga mabao mawili. Martino aliendelea kudai kuwa katika kipindi cha pili walifanikiwa kubadilisha mchezo na kucheza walivyozoea lakini walikuwa wamechelewa kwani tayari walikuwa wako nyuma. Kocha huyo amesema pamoja na kuwakosa nyota wake kadhaa kutokana na majeruhi lakini walipaswa kumiliki mpira eneo la kati kama walivyozoea kitu ambacho walishindwa kukifanya kipindi cha hivyo kukaribisha mashambulizi yaliyowaletea madhara. Pamoja na hayo kocha huyo anaamini watayafanyia kazi makosa hayo yaliyojitokeza ili kuhakikisha wanafanya vyema katika mechi zao nyingine pamoja na balaa la majeruhi linalowakabili.

No comments:

Post a Comment