Saturday, November 30, 2013

BAHRAIN GRAND PRIX KUFANYIKA USIKU MWAKANI.

MASHINDANO ya langalanga ya Bahrain Grand Prix mwakani ayanatarajiwa kufanyika usiku ili kusheherekea miaka 10 ya mashindano hayo nchini humo. Waandaaji wa mashindano hayo hivi wako katika pilikapilika za kufunga mfumo mpya wa taa ili mashindano hayo yaweze kufanyika kwa ufanisi na mafanikio. Ofisa Mkuu wa mashindano hayo nchini Bahrain Sheikh Salman bin Is Al-Khalida amesema hakuna njia nzuri zaidi ya kusherekea miaka 10 zaidi ya kufanya madereva washindane usiku. Bahrain itakuwa nchi ya pili kuandaa michuano hiyo usiku huku Singapore wao wakiwa wa kwanza kwa kuandaa mashindano hayo usiku toka mwaka 2008.

No comments:

Post a Comment