Saturday, November 30, 2013

ETO'O NJE WIKI MBILI.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amesema mshambuliaji wake Samuel Eto’o atakaa nje ya kikosi cha timu hiyo kwa kipindi cha wiki mbili baada ya kutolewa nje katikati ya wiki katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya jijini Basle. Mourinho aliwaambia waandishi wa habari kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Cameroon alipata majeraha makubwa katika msuli wa nyuma ya paja. Kocha aliongeza kuwa beki David Luiz amerejea katika mazoezi jana baada ya kuumia mguu lakini mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Southampton Jumapili itakuwa ni mapema sana kwake kucheza. Chelsea ambao wanashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi, watacheza na Southampton nyumbani kabla ya kupepetana na Sunderland na Stoke City ugenini.

No comments:

Post a Comment