Saturday, November 30, 2013

CECAFA CHALENJI: KILI KUTPA KARATA YA PILI DHIDI YA SOMALIA.

TIMU ya taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars baadae leo inatarajia kutupa karata yake ya pili kwa kucheza na Somalia katika michuano ya Kombe la Chalenji inayoandaliwa na Baraza la Michezo kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati-CECAFA. Stars ambayo inanolewa na kocha Kim Poulsen ilitoka sare ya bao 1-1 na timu mwalikwa ambayo ni Zambia hivyo ushindi katika mchezo wa leo utakuwa ni muhimu kwao ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kwenye michuano hiyo. Poulsen ambaye alilalamika tatizo la uwanja kujaa maji katika mechi ya kwanza hivyo kupelekea wachezaji wake kucheza chini ya kiwango amesema hawatapuuza mchezo wao dhidi ya Somalia ambao walibamizwa mabao 2-0 na Burundi. Katika mchezo wingine wa kundi B utakaochezwa leo Zambia watakwaana na Burundi mchezo ambao utafuata baada ya ule wa Stars kumalizika.

Picha kwa hisani ya Bin Zubery.

No comments:

Post a Comment