Monday, December 2, 2013

BASI LA PSG LASHAMBULIWA KWA MAWE.

MABASI yaliyokuwa yamebeba wachezaji wa timu za Paris Saint-Germain, PSG na Lyon yameshambuliwa kwa mawe kabla ya mchezo wa Ligue 1 baina ya timu hizo katika Uwanja wa Parc des Princes jijini Paris jana. PSG walithibitisha taarifa hizo za basi lao kushambuliwa wa mawe na kuvunjwa vioo wakati wakielekea uwanjani huku pia basi Lyon nalo linadaiwa kukutwa na tukio kama hilo. Nyota wa PSG akiwemo Zlatan Ibrahimovic, Thiago Silva na Edson Cavani wanasadikiwa kuwa walikuwemo katika basi hilo lakini hawakupata majeraha yoyote kwasababu walikuwepo katika kikosi kilichoshinda mabao 4-0 dhidi ya Lyon. Baadhi ya luninga za Ufaransa zilionyesha basi hilo jinsi basi hilo lilivyoathirika.

No comments:

Post a Comment