Monday, December 2, 2013

LAHM AANZA MAZOEZI MEPESI.

KOCHA wa klabu ya Bayern Munich, Pep Guardiola amepokea habari njema baada ya nahodha wake Philipp Lahm kuanza mazoezi binafsi. Lahm alipata majeruhi ya msuli wiki iliyopita katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya dhidi ya CSKA Moscow na kumfanya kukosa mchezo wa mwishoni mwa wiki dhidi ya Eintracht Braunschweig. Beki huyo wa kati ambaye msimu huu amekuwa akicheza katika nafasi ya kiungo hatarajiwi kuwemo katika mchezo wa katikati ya wiki dhidi ya Augsburg lakini anaweza kuwemo katika kikosi kitakachopambana na Werder Bremen Jumamosi ijayo. Bayern kwasasa wanaongoza Ligi Kuu nchini ujerumani wakiwa na alama 38 katika michezo 14 waliyocheza wakiwazidi Bayer Leverkusen wanaoshika nafasi ya pili kwa alama nne.

No comments:

Post a Comment