Tuesday, November 26, 2013

DESAILLY AWATABIRIA MAZURI IVORY COAST.

NGULI wa soka wa Chelsea, Marcel Desailly anaamini kuwa timu ya taifa ya Ivory Coast inaweza kwenda mpaka katika nusu fainali katika michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Brazil mwakani. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa alizungumza hayo wakati akiwa jijini Nairobi katika ziara na Kombe la Ligi Kuu nchini Uingereza. Desailly amesema ni jambo la kuhudhunisha kuona timu zitakazoliwakilisha bara la Afrika katika michuano hiyo karibu zote zimetokea Afrika Mgharibi na kudai kuwa Afrika Mashariki na Kusini zimeachwa nyuma kitu ambacho hakikutakiwa. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF ni lazima lihakikishe linachukua hatua za makusudi ili kukuza soka katika upande unaoonekana kuwa nyuma ili bara zima liweze kushiriki yanapokuja mashindano hayo. Akiulizwa timu anayoipa nafasi kati ya tano zilizofuzu michuano hiyo Desailly amesema anafikiri Ivory Coast wanaweza kufanya vyema na kufika nusu fainali katika michuano hiyo mwakani.


No comments:

Post a Comment