Tuesday, November 26, 2013

WENGER AKANA KUTAKA KUMSAJILI HENRY KWA MARA YA TATU.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger ameondoa uwezekano wa kumsainisha nguli wa zamani wa klabu hiyo Thierry Henry kwa mara ya tatu baada ya mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa kuanza mazoezi na timu hiyo. Henry ambaye kwasasa anacheza katika klabu ya New York Red Bull ya Marekani na kiungo wa zamani wa Arsenal Robert Pires mwenye umri wa miaka 40 wamekuwa wakifanya mazoezi na timu hiyo yenye maskani yake kaskazini mwa jiji la London ili kujiweka fiti. Henry ambaye ni mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi wakati akiwa na klabu hiyo alijiunga nao kwa mkopo Januari mwaka jana lakini Wenger amesema hana mpango wa kuchukua nyota huyo kwa mkopo tena. Wenger amesema kwasasa Henry anaruhusiwa kufanya nao mazoezi wakati akiweza na akitaka lakini sio kumsajili kwani wana kikosi kilichokamilika na kinachweza kutoa upinzani kwa timu yoyote.

No comments:

Post a Comment