Tuesday, November 26, 2013

DORTMUND HAKUNA MGOGORO - KLOPP.

MENEJA wa klabu ya Borussia Dortmund, Jurgen Klopp amekanusha kuwa timu yake iko katika mgogoro baada ya kupata vipigo katika mechi tatu mfululizo. Dortmund walianza na kipigo cha kushtusha kutoka kwa Wolfburg na baadae kuporomoka kwa alama saba mbele ya vinara wa Bundesliga Bayern Munich kwa kukubali kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa mahasimu wao hao huku wakifungwa bao 1-0 nyumbani na Arsenal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Hata hivyo, Klopp amesisitiza kuwa wachezaji wake hawajaathirtiwa chochote na vipigo hivyo mfululizo huku akitegemea kikosi chake kurejesha makali na kushinda katika mchezo wao dhidi ya Napoli baadae leo. Klopp amesema pamoja na timu yake kutofanya vyema katika mechi tatu zilizopita anaamini wachezaji wake watarejesha morali iliyopotea haswa ikizingatiwa wametoka kuzitumikia timu zao za taifa ya wengine wameshinda katika mechi zao. Kwasasa Dortmund wanashika nafasi ya tatu katika kundi F wakiwa na alama tatu nyuma ya Arsenal na Napoli.

No comments:

Post a Comment