Tuesday, November 26, 2013

TOURE ATAMBA KUIVUNJA REKODI YA MABAO YA CHELSEA.

KIUNGO wa klabu ya Manchester City Yaya Toure anaamini kuwa kikosi chao kinaweza kuvunja rekodi ya mabao ya msimu katika Ligi Kuu nchini Uingereza. Kiungo huyo mwenye nguvu amempa jeuri kocha Manuel Pellegrini juu ya uwezo wa kushambulia unaoleta matumaini ya taji kwa kusema rekodi ya Chelsea iko hatarini. Kocha Carlo Ancelotti akiwa na kikosi maridadi msimu wa 2009-2010 aliiwezesha Chelsea kufunga mabao 103 na kutwaa taji misimu minne iliyopita. Na baada ya timu ya Pellegrini kufikisha mabao 34 wakiifunga mabao 6-0 Tottenham Hotspurs Jumapili, Toure amesema lengo lao ni kuvunja rekodi hiyo.

No comments:

Post a Comment