Monday, November 25, 2013

PACQUIAO SASA AMTAKA MAYWEATHER.

BONDIA Manny Pacquiao amedai kuwa yuko tayari kupambana na Floyd Mayweather lakini ni juu ya Mmarekani huyo kusema ni lini wapigane. Pacquiao ambaye ni raia wa Philippines alipata ushindi wake wa kwanza katika miaka miwili wakati alipomtandika Brandon Rioas katika pambano la uzito wa welter kugombea mkanda wa WBO lilifanyika Jumamosi iliyopita. Bondia huyo mwenye umri wa miaka 35 amesema kazi yake ni kupigana na yuko tayari kupambana na Mayweather hivyo ni juu yake kukubali au kumuogopa kwa kukataa. Migogoro katika matangazo na masuala mengine ndio yamekuwa kikwazo kwa wawili hao kupigana.


No comments:

Post a Comment