Monday, November 25, 2013

OLYMPIQUE MARSEILLE SIO WA KUBEZA - CAZORLA.

SAFARI ya Arsenal kuelekea katika hatua ya timu 16 bora katika michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya inaweza kuonekana kama rahisi kutokana na mchezo wa nyumbani dhidi ya Olympique Marseille baadae leo lakini wameonywa kuchukulia mchezo huo kwa umakini. Arsenal ndio wanaoongoza kundi F wakiwa na alama tisa katika mechi nne walizocheza, wakiwa sambamba na Napoli waliopo katika nafasi ya pili na Borussia Dortmund waliopo katika nafasi ya pili. Kama Arsenal ikifanikiwa kuifunga Marseille na Dortmund wakishindwa kuifunga Napoli, kikosi cha Arsenal Wenger kitakuwa kimekata tiketi ya kucheza hatua hiyo huku wakiwa wamebakiwa na mchezo mmoja. Pamoja na hayo kiungo wa Arsenal, Santi Cazorla ameonya kuwa hawapaswi kudharau mchezo hata kama Marseille hawataweza kufuzu hatua hiyo. Cazorla amesema hata kama Marseille hawajapata alama yoyote katika kundi lao lakini wataufanya mchezo huo kuwa mgumu kwao kwasababu hawana cha kupoteza.

No comments:

Post a Comment