Monday, November 25, 2013

ROONEY AKIRI KUMPIGA KIATU MUTCH WA CARDIFF CITY.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Manchester United, Wayne Rooney amekiri kufanya makosa wakati alipomkwatua Jordon Mutch katika mchezo dhidi ya Cardiff City ambao walitoka sare ya kufungana mabao 2-2 jana. Mwamuzi wa mchezo huo Neil Swarbrick aliamua kumpa kadi ya njano nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 badala ya kumpa kadi nyekundu kutokana na tukio hilo. Rooney aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter akikiri kuwa baada ya kuangalia tukio hilo tena amekubali kwamba alimchezea vibaya Mutch. Naye kocha wa United, David Moyes pia alikiri Rooney kucheza faulo lakini akadai kwamba kadi ya njano aliyopewa alistahili na sio nyekundu kama wengine wanavyodai.

No comments:

Post a Comment