Monday, November 25, 2013

UZI MPYA WA BRAZIL HUU HAPA.

TIMU ya taifa ya Brazil, imezindua jezi mpya zilizotengenezwa na wadhamini wao kampuni ya Nike huku kocha Luis Filipe Scolari akitamba kuwa wako tayari kunyakuwa taji lao la sita la michuano ya Kombe la Dunia katika ardhi yao ya nyumbani mwakani. Nyota wa Barcelona, Neymar na kiungo wa Wolfsburg ya Ujerumani Luiz Gustavo ni mojawapo ya wachezaji waliopiga picha kuzitangaza jezi hizo mpya katika ufukwe maarufu wa Copacabana. Scolari amezionya timu pinzani katika michuano hiyo kwamba wapo tayari kuhakikisha wanaweka historia mpya kwa kunyakuwa taji hilo kwa mara ya sita. Kocha huyo pia alisifu mwonekano mzuri wa jezi hizo na kutania kuwa kilichokosekana katika jezi hizo ni nyota sita akimaanisha idadi ya mataji ya michuano hiyo waliyochukua. Uzinduzi wa nembo ya 2014 ni mwanzo wa kampeni za Nike ambapo jezi ya Brazil ndiyo huwapatia mauzo makubwa kimataifa.

No comments:

Post a Comment