Monday, November 25, 2013

MARK WEBBER ATAKUMBUKWA DAIMA KATIKA LANGALANGA - ALONSO.

DEREVA wa mashindano ya langalanga, Fernando Alonso amedai kuwa wapenzi wa mashindano hayo watamkumbuka Mark Webber kufuatia dereva huyo wa Red Bull kuamua kustaafu. Webber ambaye ni raia wa Australia alikamata nafasi ya pili katika mashindano ya Grand Prix ya Brazil nyuma ya dereva mwenzake wa Red Bull Sebastian Vettel pamoja na rafiki yake wa karibu Alonso ambaye alimaliza katika nafasi ya tatu. Alonso ambaye ni dereva wa Ferrari amesema hawezi kusahau mashindano hayo ya Brazil jinsi walivyokuwa wakishindana ndio maana watamkumbuka siku zote. Mbali na Alonso nyota mwingine wa langalanga aliyetoa heshima zake kwa Webber ni pamoja na bingwa mara nne wa dunia wa michuano hiyo Vettel ambaye amedai kuwa watamkosa mmoja wa madereva hodari na mwenye haiba ya kipekee.

No comments:

Post a Comment