Friday, November 22, 2013

FAINALI ZA KLABU BINGWA YA DUNIA ZITAKUWA BORA,

ZIKIWA zimebaki wiki mbili kabla ya kuanza kutimua vumbi kwa michuano ya Klabu ya Bingwa, rais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Sepp Blatter anaamini kuwa wenyeji Morocco wako tayari kwa ajili ya michuano hiyo. Blatter amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea hatua za mwisho za maandalizi ya michuano hiyo pamoja na timu zitakazoshiriki. Rais huyo amesema timu zitakazoshiriki michuano hiyo ni pamoja na Guangzhou Evergrade ya China ambao ni mabingwa wa Ligi ya Mabingwa barani Asia, Bayern Munich mabingwa wa Ulaya na Al Ahly mabingwa wa Afrika. Wengine ni Auckland City mabingwa Oceania, Monterrey mabingwa wa CONCACAF, Atletico Mineiro mabingwa wa Amerika Kusini na Raja Casablanca ambao wameingia katika michuano hiyo kama wenyeji.

No comments:

Post a Comment