Friday, November 22, 2013

ZIDANE ALIKUWA BORA KULIKO MESSI - PELE.

NGULI wa soka wa zamani wa Brazil, Pele amedai kuwa Zinedine Zidane alikuwa mchezaji bora kuliko alivyo Messi wakati akiwa katika kiwango cha juu lakini akabainisha kuwa angemchagua nyota huyo wa Barcelona badala ya Cristiano Ronaldo katika tuzo za Ballon d’Or. Zidane alifanikiwa kushinda taji la Kombe la Dunia na Ulaya wakati akiitumikia Ufaransa kipindi hicho pamoja na taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na baadae Ballon d’Or wakati akiwa anacheza klabu ya Real Madrid. Pamoja na kwamba wadau wengi wa soka wakidai kwamba Messi ni mmoja wa wachezaji bora kabisa kuwahi kutokea akiwa ameshinda tuzo ya Ballon d’Or mara nne mfululizo, Lakini Pele ana mawazo tofauti kuhusiana na hilo. Pele amesema kwa juhudi binafsi anadhani Zidane alikuwa bora kuliko Messi, na ukilinganisha wachezaji aliokuwa akicheza nao kipindi hicho huwezi kuwalinganisha kwa kiwango sawa na wachezaji anaocheza nao Messi kama Xavi Hernandez na Andres Iniesta. Pele aliendelea kudai kuwa pamoja na hayo angemchagua Messi kushinda tuzo ya Ballon d’Or badala Ronaldo kwasababu ya mbinu za hali ya juu alizonazo anapokuwa uwanjani.

No comments:

Post a Comment