Tuesday, November 19, 2013

DESCHAMPS HAPASWI KULAUMIWA KAMA UFARANSA IKISHINDWA KUFUZU - PLATINI.

RAIS wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA, Michel Platini anaamini kuwa kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps hatalaumiwa kama nchi hiyo ikishindwa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika Brazil mwakani. Ufaransa ina kibarua kigumu katika mchezo wao wa mkondo wa pili hatua ya mtoano utakaochezwa baadae leo baada ya kufungwa mabao 2-0 na Ukraine wiki iliyopita, lakini Platini amesisitiza kuwa ni jukumu la wachezaji kupambana kuhakikisha wanapata nafasi ya kwenda Brazil. Platini amesema siku zote amekuwa akiwaunga mkono makocha wa Ufaransa hivyo kwa maono yake hadhani kama kocha anapaswa kuwajibishwa kama nchi hiyo ikishindwa kufuzu kwani ni jukumu la wachezaji kuhakikisha wanageuza matokeo ya wiki iliyopita ili waweze kufuzu. Deschamps alikuwepo katika kikosi cha Ufaransa enzi hizo akiwa mchezaji wakati waliposhindwa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia mwaka 1994 baada ya kupoteza mechi zake za mwisho dhidi ya Israel na Bulgaria.

No comments:

Post a Comment