Tuesday, November 19, 2013

FABREGAS AANZA MAZOEZI.

KLABU ya Barcelona imesema kuwa kiungo wake mahiri Cesc Fabregas amerejea tena mazoezini huku akiendelea kupona maumivu ya mguu yanayomkabili. Fabregas aliumia kisigino cha mguu wake wa kulia katika ushindi wa mabao 4-1 waliopata dhidi ya Real Betis Novemba 10 na kusababisha kuondolewa katika kikosi cha Hispania kilichokuwa kikijiwinda na mechi za kimataifa za kirafiki dhidi ya Equatorial Guinea na Afrika Kusini. Mbali na Fabregas nyota wengine walio majeruhi Gerard Pique na Jordi Alba wameendelea kufanya mazoezi mbali na wachezaji wenzao wakati nao wakiendelea kupona taratibu. Mabingwa hao wa La Liga ambao hawajafungwa mpaka sasa wataikaribisha Granada Jumamosi huku wakiongoza La Liga kwa tofauti ya alama tatu mbele ya Atletico Madrid wanaoshika nafasi ya pili baada ya kucheza mechi 13.

No comments:

Post a Comment