Tuesday, November 19, 2013

RAGE ANG'OLEWA SIMBA, WAMO PIA JULIO NA KIBADEN.

KAMATI ya Utendaji ya klabu ya Simba, imemsimamisha mwenyekiti wake Ismail Aden Rage kwa madai ya kukiuka miiko ya uongozi pamoja na katiba ya klabu hiyo. Hatua hiyo inakuja ikiwa ni siku moja baada ya Rage kuwasainisha mkataba wachezaji wawili kutoka Zanzibar Ally Badru na Awadh Juma aliyekuwa anacheza Mtibwa. Taarifa ya awali inadai kuwa Rage amekuwa hajishughulishi kwa karibu na timu hiyo lakini pia amekuwa akikiiuka baadhi ya mambo ndani ya katiba na ndio maana kamati ya utendaji imepata nguvu ya kumsimamisha kwenye kikao walichokaa jana. Maamuzi juu ya hatma ya Rage yatatolewa katika Mkutano Mkuu wa klabu hiyo unaotarajiwa kufanyika Desemba mosi mwaka huu. Mbali na Rage lakini pia kamati hiyo ilivunja benchi lote la ufundi la timu hiyo lililokuwa likiongozwa na kocha mkuu Abdalah Kibaden na msadizi wake Jamhuri Kihwelu maarufu kama Julio. Nafasi ya Kibaden sasa itashikiliwa na kocha wa zamani wa Gor Mahia, Zdravko Logarusic ambaye ni raia wa Croatia ambaye atakuwa akisaidiwa na aliyekuwa kocha wa kikosi B cha klabu hiyo Seleman Matola. Kocha huyo anatarajiwa kutua nchini Desemba mosi na moja kwa moja kuanza maandalizi ya msimu ujao siku inayofuata.

No comments:

Post a Comment