Monday, November 18, 2013

HAYE ASHAURIWA KUSTAAFU MASUMBWI BAADA YA KUFANYIWA UPASUAJI.

BINGWA wa dunia wa zamani wa ngumi za uzito wa juu, David Haye ameshauriwa kustaafu mchezo huo baada ya kufanyiwa uapsuaji mkubwa wa bega. Haye mwenye umri wa miaka 33 raia wa Uingereza alifanyiwa upasuaji huo uliochukua saa tano katika bega lake la kulia huko nchini Ujerumani Alhamisi iliyopita. Bondia huyo ambaye alifuta pambano lake na Tyson Fury lililokuwa lifanyike Februari mwakani, amesema amekuwa akiokea ushauri kutoka kwa wadau wa mchezo huo kwamba wakati wake wa kustaafu umefika. Kama akiamua kustaafu itakuwa ni mara ya pili kwa Haye baada ya kufanya hivyo Octoba mwaka 2011 miezi mitatu baada ya kupoteza mkanda wake wa WBA kwa Wladimir Klitscho wa Ukraine katika pambano lilofanyika Ujerumani.


No comments:

Post a Comment