Friday, November 29, 2013

DRC KUTEUA KOCHA MPYA KABLA YA CHAN.

SHIRIKISHO la Soka la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limethibitisha kutaja jina la kocha mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo kabla ya michuano inayokuja ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani yatakayofanyika nchini Afrika Kusini. Nchi imekuwa bila kocha toka alipoondoka Mfaransa Claude Le Roy ambaye aliondoka baada ya kushindwa kuiwezesha timu hiyo kufuzu hatua ya mtoano katika kusaka tiketi ya Kombe la Dunia 2014. Mwenyekiti wa shirikisho hilo Constant Omari alithibisha hilo na kudai kuwa watateua kocha mpya Desemba au mapema Januari kabla ya kuanza michuano hiyo. DRC ambao wameshinda michuano hiyo mwaka 2009, walikata tiketi baada ya kuiondosha Cameroon katika mechi za kufuzu.

No comments:

Post a Comment