Friday, November 29, 2013

SIOGOPI KUPANGWA NA REAL MADRID WALA BARCELONA - PELLEGRINI.

MENEJA wa klabu ya Manchester City, Manuel Pellegrini amesema haogopi kupangwa pamoja na timu kati ya Barcelona au Real Madrid katika hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Kikosi cha Pellegrini tayari kimefuzu hatua ya makundi lakini wanaweza kumaliza katika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa watetezi Bayern Munich ambao watacheza nao katika mechi ya mwisho katika hatua ya makundi. Hata hivyo, Pellegrini ambaye ni raia wa Chile amesema hawatakuwa na uoga kwa yoyote watakayepangwa nae katika hatua ya timu 16 bora na anaamini kuwa timu zingine nazo hazitataka kukutana na City. Pellegrini amesema Hispania ina timu ngumu haswa Barcelona na Real Madrid lakini pia Atletico Madrid nao wamekuwa na msimu mzuri lakini alitamba kuwa hawamuogopi yoyote watakayekutana naye kwasababu anaamini ana kikosi imara.

No comments:

Post a Comment