Friday, November 29, 2013

HATUNA MPANGO WA KUHAMISHA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA 2014 NJE YA BRAZIL.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter amedai kuwa hawana mpango wa kuhamisha michuano ya Kombe la Dunia 2014 nje ya Brazil pamoja na tukio lilitokea wakati wa maandalizi ya michuano hiyo itakayochezwa kipindi majira ya kiangazi. Watu wawili walifariki baada ya crane kuanguka na kuharibu sehemu ya Uwanja wa Corinthians Arena uliopo jijini Sao Paulo. Brazil inatarajiwa kucheza mchezo wake wa ufunguzi katika uwanja huo wenye uwezo wa kuingiza watazamani 65,000 katika siku zisizozidi 200. Pamoja na tukio hilo Blatter ameendelea kusisitiza kuwa hakuna mpango mwingine wowote kuhusiana na michuano hiyo kwasasa. Serikali ya Brazil imekiri kufanya jitihada ili kukamilisha viwanja 12 vitakavyotumika kwa ajili ya michuano hiyo lakini mpaka sasa ni viwanja sita pekee vilivyokuwa tayari huku vingine sita vilivyobakia vikiwa bado kumalizika.

No comments:

Post a Comment