Friday, November 29, 2013

LAHM NJE WIKI MBILI KWA MAUMIVU YA MSULI.

NAHODHA wa klabu ya Bayern Munich, Philipp Lahm anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki mbili baada ya kuumia msuli wa paja katika ushindi wa mabao 3-1 iliyopata timu yake dhidi yake dhidi ya CSKA Moscow Jumatano iliyopita. Lahm mwenye umri wa miaka 30 alifanyiwa vipimo wakati timu hiyo iliporejea jijini Munich na anatarajiwa kukosa mechi mbili zijazo za Ligi Kuu nchini Ujerumani maarufu kama Bundesliga. Katika taarifa iliyotolewa katika mtandao wa klabu hiyo, Lahm atakosa mechi kati ya Bayern dhidi ya Eintracht Braunschweig utakaochezwa kesho na pia mchezo dhidi ya Augsburg. Mbali na Lahm, Bayern pia itawakosa nyota wake wengine kutokana na majeruhi wakiwemo Bastian Schweisteiger, Franck Ribery, Claudio Pizarro na Xherdan Shaqiri.

No comments:

Post a Comment