Friday, November 29, 2013

PAMOJA NA KUGONGA 40 MKONGWE GIGGS BADO ANATAKA KUENDELEA KUCHEZA.

KIUNGO mkongwe wa klabu ya Manchester United, Ryan Giggs hana mpango wowote wa kutundika daluga pamoja na kufikisha umri wa miaka 40 leo. Kiungo huyo wa kimataifa wa Wales amekuwa akiitumikia klabu hiyo yenye maskani yake Old Traford kipindi chote akiwa amecheza mechi 953 toka alipocheza katika kikosi cha kwanza cha United kwenye mechi dhidi ya Everton mwaka 1991. Giggs amesema anajisikia mwenye bahati kucheza katika klabu moja kwa kipindi chote hicho huku akiwa amezungukwa na wachezaji na pamoja na kocha mzuri. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa ingawa kunakuwa na vipindi vigumu muda mwingine lakini bado anafurahia kuwepo hapo kwa kipindi kirefu kadri kiwango chake kitakavyomruhusu. Amesema kama angekuwa anahama kutoka klabu moja kwenda nyingine angekuwa ameshakwisha hivi sasa kama ilivyo kwa wenzake walioanza pamoja kama David Beckham, Paul Scholes, Nick Butt, Gary Neville na Phill Neville.

No comments:

Post a Comment