Friday, November 29, 2013

UEFA YAMLIMA ADHABU YA MECHI TATU MBOKANI KWA KUMTUKANA MWAMUZI.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC, Dieumerci Mbokani ametwangwa adhabu ya kufungiwa mechi tatu na Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA baada ya kukutwa na kosa la kumtukana mwamuzi. Katika taarifa yake UEFA imesema Mbokani mwenye umri wa miaka 28 anayekipiga klabu ya Dynamo Kyiv alitumia maneno yasiyo ya kiungwana kwa mwamuzi wakati wa mchezo wa makundi wa michuano ya Europa League mapema mwezi huu. Dynamo Kyiv ilithibitisha adhabu hiyo jana lakini hawakuweka wazi kama wataka rufani kupinga adhabu hiyo kwa mchezaji wao. Mbokani amecheza misimu mitatu katika klabu ya Anderlecht ya Ubelgiji, akicheza mechi 53 na kufunga mabao 34.

No comments:

Post a Comment