Thursday, November 28, 2013

TANZANIA YAKWEA VIWANGO FIFA.

TANZANIA imekwea kwa nafasi tano katika viwango vya soka vinavyoandaliwa kila mwezi na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA. Mwezi uliopita Tanzania ambayo imekuwa ikishuka na kupanda katika viwango hivyo iliporomoka mpaka nafasi ya 129 lakini katika viwango vilivyotolea leo imepanda tena mpaka katika nafasi ya 124. Kwa upande wa Afrika Ivory Coast imeendelea kuongoza kwa kushika nafasi ya 17 katika viwango vya dunia ikifuatiwa na Ghana waliopo katika nafasi ya 24 huku Algeria wakiwa nafasi ya tatu kwa kushika namba 26. Wengine ni Nigeria waliopo nafasi ya 36 na tano bora kwa upande wa Afrika inafungwa na Misri waliokwea kwa nafasi 13 moaka nafasi ya 38 katika viwnago hivyo.


No comments:

Post a Comment