Thursday, November 28, 2013

WAWILI WAFA KATIKA AJALI KWENYE UWANJA WA KOMBE LA DUNIA BRAZIL.

WATU wawili wamekufa katika ajali kwenye moja ya viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil mwakani. Vifo hivyo vimetokea wakati crane lilipoanguka na kuharibu sehemu ya Uwanja wa Corinthians Arena uliopo jiji Sao Paulo nchini humo. Brazil inatarajiwa kucheza mechi yake ya ufunguzi wa michuano hiyo katika uwanja huo wenye uwezo wa kuingiza watu 65,000 Juni 12 mwakani. Msemaji wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA amesema waandaaji wa michuano hiyo watafanya uchunguzi wa kina kuhusiana na tukio hilo huku rais wa shirikisho hilo akituma salamu zake za rambirambi kwa ndugu waliofiwa na jamaa zao.

No comments:

Post a Comment